Sunday, October 11, 2015

SIR HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI 18

SIRI HUFICHULIWA NA UJASIR WOGA UKIKITHIRI 18
SEHEMU YA 18

Irene alisita kidogo na alipoangalia watu wote katika hoteli hiyo waliduwaa wakiwaangalia wao kwa kuepusha aibu Irene ilibidi aeleweke tu na kusema haya nimekusamehe simama sasa , ahsante alijibu Adam ambaye aliposimama hakusimamam hivi hivi bali alijifanya kajisahau na kumkumbatia Irene ambaye naye kwa kuwa ni mbele ya watu aliweka mikono yake mgongoni mwa Adam na kumkumbatia huku Adam kakamatilia kiuno daaah huyu jamaa kweli ngombe hazeeki maini yani tabia zake zilikua zile zile kwa vijana wa sasa wangemuita kicheche , kisha wakakaa tena kwenye meza yao na Adam akaanza maongezi yake tena kwa Irene na kumwambia , ahsante kwa kunisamehe kisha naweza kujua mwanangu sa hivi yuko wapi na anaitwa nani , kwa hilo siwezi kukwambia kwa sasa ila naomba please please usidhani eti kukusamehe ndio mambo yako sawa hapana kwanza hapa una bahati sana na shukuru Mungu leo sijui nimeamkia wapi tu haya mi naomba niende sasa , aaah si nikupe lifti hadi kwako hata nipajue , hapana sitaki sitaki siku nikitaka upajue utapajua kwa sasa nitakachoweza kukuhakikishia ni urafiki tu mengine yote hapana, aaah masharti magumu hayo sawa mama nimekuelewa alisema Adam nakuagana kila mmoja akaenda kwake , Kesho ya muda wa mchana Adam alishangaa kumuona Irene katika viunga vya kampuni ya TBL mawazo yake yote yalimtuma anakuja kumtafuta yeye kumbe Irene alikuja kumuumiza zaidi Adam aliyefikiri kasamehewa hivi hivi tu kirahisi rahisi , Irene alikuja kumuona Humphrey , Adam si akatoka anajiamini kwamba Irene anakuja kwake kwa mbwembwe huku akitabasamu tabasamu kabla hajafika Irene alipokua Irene si akanyoosha mikono kama mtu aliyekua akihitaji kumkumbatia mtu fulani Adam si akazani ni yeye naye akanyoosha mikono kama anataka kumkumbatia Irene mara ghafla akatokea mtu nyuma yake Adam na kwenda kukumbatiana na Irene alikua ni Humphrey daaah Adam ilimuuma sana hii ilikua ni michezo ya kitoto ikichezwa na watu wazima hahahahahaha hayo ndio mapenzi bwana hayakui yani michezo ya kitoto mtu mzima anamfanyia mtu mzima mwenzake , huku napo sio pa kusahau kwani siku hii ndio haswa ile siku mjenzi alikua anakabidhiwa vifaa vyake vya kazi aanze kazi ilikua ni kazi ya kukimbiza mwenge yani namaanisha ilikua siku ya kuvunja ahadi ya siku nyingi waliowekeana ni hawa vijana wa kizazi kipya Vatican na Martha ndio hasa walikutana tena baada ya kutoonana kwa muda mrefu sasa nao waliona ulikua ni muda bora wa kupinga amri za Mungu kwa kuvunja mojawapo ya amri zake ambayo ilikua ni amri ya sita. Hawaanzagi hivi hivi bali ndani ya jiji la miamba miamba la Mwanza vijana hawa wawili walikutana katika hoteli ya Golden crest kupata maraha ya dunia yani duu yani daah Vatican kishamchomoa mama yake kama laki mbili hivi za kutumia siku hiyo mtoto mwenyewe mmoja huyo chochote atakacholilia anapewa haikua shida kupewa laki mbili na mama haya tuendelee, baada ya vinywaji na chakula hotelini hapo sasa ulikua ni muda wa kupumzika . Katika chumba walichokua Martha alienda kwanza kuoga humo humo bafuni na Vatican kwa haraka haraka zake alikua tayari ameshajiaandaa yani kabaki na nguo kama tatu mwilini mwake ambazo zilikua ni kaptula fupi na nguo ya ndani kisha na kaushi wakati akiwa anasubiria kwa hamu kumwaga marhamu harufu marashi ya utamu sogea wote tule humu Vatican aliweka kwenye redio wimbo wa Whitney Houston I will always love you Martha alitoka nao taratibu bafuni akiimba wimbo huo bila ajizi akaumwaga mchuzi mbele ya walowezi ni kile ki taulo alichokua amekivaa alikiachia kikaanguka hadi chini pwaaa mambo hadharani karibu mwandani tuonyeshane vya ndani mimba hiyo ajali kazini hebu karibia tusafishe nyota kila siku niwe ninakuota ilikua ni katika chumba kimoja kitanda kimoja watu wawili wakiwa na wazo moja na wakifanya tendo moja kwa pamoja huku hawajui kama ni wa baba mmoja aisee hatutapoteza sana muda huko wewe kama mtu mzima ulishajua nini kilichoendelea hahahahaha jiongeze mkubwa hayo ndio yaliyoendelea huko

0 comments:

Post a Comment