Sunday, October 11, 2015

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI 21

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
SEHEMU YA 21

Dayness kwa Irene kwamba ndio mke wake na Dayness hakusita kumuomba msamaha Irene kwa kitendo alichomfanyia , Dada samahani sana naomba radhi jana kwa mambo niliyokufanyia , usihofu dada hakuna tatizo, wote wakakaa na kujumuika pamoja kwa chakula cha jioni hapo walipiga stori na kubadilishana mawazo kila mtu akiwa na mwanamke wake ila kumbe ule ulikua ni mpango wa Adam kumweka sawa mke wake Dayness na aache wivu wake Ila pia taarifa mbaya kwa Adam zilikua ni hizi siku hiyo ni pale Humphrey alipopiga magoti chini na kutoa kiboksi kilichokua na pete ndani yake akiwa amemshika mkono Irene na kuelekeza kabisa pete ile karibu na kidole cha Irene huku akisema maneno haya , Irene will you marry me , Irene alikaa kimya kidogo kumuangalia Adam alikua ameinamisha kichwa chini huku kamshika mkono mke wake kisha baada ya kufikili kidogo Irene alikisogeza kidole chake hadi kikatosha kabisa kwenye ile pete na akajibu ndiyo huku akimnyanyua na kukumbatiana na Humphrey, kweli mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu aisee Adam aliumia sijapata kuona hadi mke wake akashitukia kidogo, kisha wakiwa na furaha huku wakiwa wamekumbatiana na kushikana mikono Humphrey na Irene walishitushwa na kauli ya rafiki yao Adam alipoaga na kuomba eti awaache wafurahie siku yao hahahaha kweli mpenzi yanaumiza Adam aliumia sana kuendelea kukaa pale hivyo aliona bora aondoke asiendelee kuumia pia kitu hicho kilikua nje ya mpango wao na Humphrey hivyo aliona Humphrey kama amemsaliti kwenye mpango waliopanga na njia pekee ilikua kuondoka na kuumia mwenyewe nyumbani kweli alimchukua mke wake wakaaga na kuondoka , Humphrey yeye kwake furaha tupu na kisha akaagana na Irene wakaachana.Irene alipokua peke yake aliwaza na kujua kuwa alikua anachezea tu hisia za Humphrey ili kumuumiza Adam kweli dunia hii unaweza hata ukamuoa mwanamke na kuishi naye na mkazaa naye kumbe hakupendi alifanya hivyo tu kumuumiza mtu mwingine ambaye aidha ni mtu wa karibu yako sana na anawaona na anaumia sana ndivyo mzunguko wa maisha ulivyo na watu baadhi hupitia huko. Adam aligeuka na kuwa kama chizi sasa nadhani alifunga ndoa na baa kabisa kwani Adam alikua mlevi wa kupindukia alirudi usiku wa manane upendo tena kwa mke wake uliisha kabisa hata mtoto wake tu Martha hakumjali yani alichanganyikiwa hata sijui mfano wake nisemeja kazini aliacha kwenda na siku moja Humphrey alimtembelea kumpa kadi ya harusi yake nadhani hapo ndipo Adam alipotaka kufa kabisa Dayness aligundua kuwa mume wake hakuwa sawa na mwanamke mwenye mapenzi mema na mume wake hutafuta chanzo cha tatizo na kuiokoa ndoa yake hata kwenye biblia imeandikwa mwanamke mwerevu huiokoa ndoa yake bali mpumbavu huiangamiza , basi Dayness alikwenda na wazo la kuiokoa ndoa yake aliwaza aende kukutana na Irene na kuongea naye kwani alihisi kuwa Irene alikua chanzo cha mume wake kuwa hivyo . Kweli Dayness alifika nyumbani kwa Irene na alikaribishwa na Vatican , hakujua kwamba Vatican alikua mpenzi wa mtoto wake Martha. 

0 comments:

Post a Comment