SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
SEHEMU YA 15
Mary hakuwa na uwezo wa kutunza siri aliwapigia
simu wazazi wake na Martha na kuwaeleza ukweli wote mzee Adam alikasirishwa
sana na Kufunga safari kwenda Dar akiwa na mke wake Dayness walipofika
wakakutana na mtoto wao kitu cha kwanza kabla ya salamu Martha alipokea kibao
kutoka kwa baba yake mzee Adam , mama yake alijaribu kumtetea na kisha akaenda
naye chumbani na kumwacha mzee Adam na Mary wakiwa nje mzee Adam alimpongeza
Mary kwa kazi nzuri ya kutoa taarifa huko ndani napo mama yake Martha
alimwamuru Martha avue nguo zote na kuanza kumkagua kwa kuwa yeye alikua mzoefu
alijua kila kitu na akajua kuwa Martha alikua hajafanyiwa chochote na kumwambia
mwanae , Martha pole sana mama kwa kibao kutoka kwa baba usichana wako bado
unao usihofu mama ukufanywa chochote , kweli mama , kweli usihofu acha
nikaongee na baba we kaa hapa sawa , sawa, alipotoka akamwita mzee Adam na
kumwambia baba Martha Martha bado , umejuaje, mi nimeenda nikamkagua bado ipo ,
usije ukawa unamtetea mwanao , haa twende mwenyewe ukaone kawa unadhani
nakutania , basi acha nakuamini sana mke wangu sa sijui nitamwambiaje wivu
kweli na kile kibao ila lazima nimpeleke akasome boarding siku nyingine
watamfanya kweli hebu niitie Martha alikuja huku akiogopa ogopa kisha mzee Adam
akamwita na kumwambia Sikia Mama pole kwa
kukuumiza ila hiki nitakachokwambia kitakuumiza zaidi nataka nikuamishe kabisa
hapa na ukasome shuleni boarding, baba jamani mbona unanionea hivyo mi sipendi
boarding maisha ya huko magumu sana , sasa nataka ujue maisha magumu yalivyo
kuanzia leo utahamia bodying. Kweli uamuzi ukitolewa na mzazi tena baba huwezi
kupinga ndio ilivyotokea kwa Martha alikubali na
kupelekwa shule boarding hapo hapo shuleni kwao ila baada ya siku kadhaa hivi
Vatican alikwenda alipokua anaishi Martha na ndugu yake Mary kufika pale jamaa
alienda kajiandaa ile mbaya maua, chocolate. Kadi ya sorry vyote alibeba kama
ishara ya upendo na kuja kuomba msamaha alipofika akakutana na Mary
akamkaribisha ndani kisha alipomuulizia Martha, Mary alikaa kimya kidogo na
kumwambia Martha hayupo kahamishiwa boarding shuleni , (kama akishituka hivi)
boarding kwa nini, we si ulimfanyia vibaya heheheee halafu kumbe hakuna kitu ,
Mary Kumbe naye alikua anamtamani tamani Vatican akaanza kumwambia huku akaja
kukaa karibu naye na kuanza kuvuta vuta sketi yake fupi , hivi we Vatican huoni
wanawake wa kupenda yani unahangaika na Martha mtoto huyo analialia na
kukusumbua hivi hutuoni (huku akinyanyuka na kujigeuza mbele nyuma kama anamuonesha
Vatican umbo lake) umeona mambo hayo cheki mtoto ninavyolipa eleweka wewe
utaendelea hadi lini kulala na chakula halafu una njaa unaacha kula kisa hujui
cha nani au unaogopa funguka mtoto wa kiume nipo hapa kwa ajili yako sema sasa
(huku akipitisha mkono wake shingoni mwa Vatican), aaah Mary acha kwanza basi
tufanye hivi hebu chukua hivi . Akampa maua kadi na ile choclate Mary alifurahi
akajua labda Vatican kishanasa kwenye mtego wake kumbe wapi mawazo ya Vatican
bado yapo kwa Martha tu kisha Vatican alimuaga Mary na kumpoteza zaidi si
akamkumbatia basi Mary kichwa hilo kajua ndege mjanja yupo kwenye tundu bovu
kumbe wapi. Vatican alifuatilia hadi akampata mtu aliyekua anasoma st marrys
day aliyeitwa Angel. Angel alikua anasoma darasa moja na Martha , Vatican
alimtuma Angel akamsalimie tu Martha , Martha alipopata habari hizo moyo
ulilipuka ila naye alikua kaanza kumpenda Vatican hata ile hasira aliyekua nayo
kwa Vatican ilitoka alipojua kuwa Vatican hakufanya chochote basi mind game
ndio ilifanya kazi hivyo Martha alitokea kumpenda sana Vatican kisha alimpa
majibu Angel na kumwambia Akamwambie Vatican aandike barua kwa kuwa shule
hawakuruhusiwa kuwa na simu kweli Vatican aliandika barua na kumpa Angel na
ilisomeka kama hivi " mambo natumaini we ni mzima wa afya pole na samahani
kwa niliyokutendea najua nilikuudhi sana ila naomba nikwambie ukweli nilipolala
na wewe sikufanya chochote wala sikulala na wewe usiku mzima bali nilikuja tu
asubuhi naomba unisamehe kwa kukuchezea akili nakutakia masomo mema love you.
Ndani ya barua yake Vatican aliweka chocolate kama ishara ya kumvutia Martha.
Martha naye hakusita kujibu barua hiyo na kuandika hivi Kwako kipenzi Vatican najua kuwa nilikua na hasira kwako ila hilo ilikua
ni sababu nilihisi umenitendea matendo mabaya ila haikua hivyo nimeamini kuwa
we ni muaminifu na unanipenda kweli nachukua nafasi hii kukuambia kuwa
nimekubali kuwa mpenzi wako kuanzia leo ila kwa masharti haya matatu kwanza
sitopenda tukutane kimwili hadi nimalize kidato cha nne pili sipendi kuumizwa na nitajiua
nikigundua una mpenzi mwingine hivyo nataka uwe wangu peke yangu tu hilo muhimu
sana kisha sitopenda nifahamike sana kwa rafiki zako kuwa mi ni mpenzi wako
naomba kwa sasa iwe siri ahsante kwa chocolate dedication massari real love i
love you .
Wednesday, October 07, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment