Sunday, October 11, 2015

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIR WOGA UKIKITHIRI 20

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
SEHEMU YA 20

Dayness aliyekua anamfuatilia mume wake kuwa wapi hua anakwenda ili ajue ni nani anayemuharibia mume wake hadi mapenzi yao yanapungua alifika , alipofika tu hakuamini alichokiona machoni kwake Dayness hakuweza kuizuia hasira yake na kumpalamia Irene kwa vibao na magumi Adam alijitahidi kumzuia sana Dayness asimfikie wala kumuumiza Irene ila alichoharibu zaidi ni pale Adam alipomshikilia Irene badala ya mke wake Dayness hapo ndipo Dayness alipatwa na hasira zaidi na kuondoka katika maeneo hayo Adam alimuomba Irene radhi na kumkimbilia Dayness. Dayness alikimbia kwa haraka kwenye gari lake na kuondoka Adam naye hakusita kumfuatilia mke wake hadi nyumbani .Dayness aliendesha gari ovyo sana wakati akienda nyumbani nusura amgonge mtoto wa shule kwa mwendo kasi aliokua nao ila akamkwepa na yeye kwenda kugonga nguzo ya umeme iliyokua kandokando ya barabara , kama uliwahi kusikia mapenzi yanaua na ukajiuliza maswali mengi sana ni kivipi mapenzi yanaua basi hii ndio njia mojawapo ya mapenzi yanavyoua. Mungu saidia Dayness akatoka mzima wa afya haraka alikimbia na kulitelekeza gari lile na kupanda daladala alipofika nyumbani kila kitu kilichokua mbele yake alikitupa na kuharibu haribu kisha akaenda chumbani na kuweka nguo zake zote akiwa aliye dhamilia kuondoa ila akiwa anaendelea Adam akafika , Mke wangu mke wangu Dayness sikiliza basi mke wangu eeeh nisikilize basi usije ukajutia baadae maamuzi unayoyafanya na kumuumiza mtoto wetu Martha hebu nisikie basi , Dayness aligeuka huku akilia na amsikilize Adam anasema nini na Adam akaendelea , ulichokiona mama Martha sio unavyofikilia huyo ni Irene mwalimu wa Martha wa kitangiri pia ni mpenzi wake Humphrey yule rafiki yangu kipenzi sasa hapo alikua ananielezea kuhusu ugomvi wao na Humprey sasa nikawa nampa pole ndio wewe ukaja hebu fikiri ni miaka ishirini na kadhaa tupo pamoja sasa sijawahi kukudanganya wala kukuumiza iweje leo unifikilie vibaya au hatuaminiani mke wangu siku hizi , Dayness huku akifuta machozi alikua kama aliyeridhika na jibu la mume wake na kwa upole akajibu, basi sawa mi nilijua labda ndio umeniacha sababu siku hizi sikuelewi kabisa haki yangu ya ndoa hunipi salamu imekua tabu au tuna ugomvi, hapana hapana mke wangu ni matatizo madogo madogo yalinipata kazini ndio maana nilikua hivyo , sasa mimi si ni mke wako unashindwa nini kuniambia matatizo yako tukasaidiana, eeeeeeeh basi basi mke wangu usihofu hayo matatizo madogo sema sasa au twende sa hivi eeeh mke wangu , mmmh kukwambia tu tayari ulishataka, si umeomba mwenyewe , we naye huzeeki , aaah wapi ng'ombe hazeeki maini wewe sema kama upo tayari , haya basi sawa njoo. Ugomvi huo ulisha hivyo na Adam akafanikiwa kuiokoa ndoa yake kwa muda kisha kesho yake alimwelezea rafiki yake Humphrey yaliyomkuta kisha Humphrey aliwaalika Adam na Dayness kwenye chakula cha jioni huku yeye akiwa amemualika Irene wote walikutana kwenye meza moja na kusalimiana kwa pamoja kabla hawajaendelea Adam alichukua nafasi hiyo kumtambulisha Dayness kwa Irene kwamba ndio mke wake na Dayness hakusita kumuomba msamaha Irene kwa kitendo alichomfanyia.

0 comments:

Post a Comment