Friday, October 09, 2015

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI 16

                  SIRI  HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
                                              SEHEMU YA 16

ahsante kwa chocolate dedication massari real love i love you . Hayo ndiyo ya moyoni ya Martha aliyoyatoa kwa Vatican. Vatican alipoipokea tu barua kutoka kwa Angel na kuisoma nusu alie alipiga makelele hayo kama mwanafunzi wa form four aliyepata matokeo kuwa kafaulu wakati asilia 80 wamefeli utani tu ila ki ukweli Vatican alikua mwenye furaha sana pia furaha hiyo iliongezeka zaidi pale Vatican alipofaulu kwenda mwaka wa tatu kwa ufaulu mkubwa wa GPA ya nne na hakusita kumshirikisha mama yake katika furaha yake ilikua kama kuokota dhahabu mchangani huku wengine wanahangaika kuchimba migodini . Shikamoo mama , marahaba hali yako ,nzuri , za masomo , nazo nzuri , vipi unataka shilingi ngapi sababu nishazoea ukinipigia tu wewe unaomba hela , haaaa mama sio hivyo leo nitabadilisha ratiba kidogo nina jambo jema nataka kukwambia mama yangu nimefaulu kwenda mwaka wa tatu tena kwa GPA kubwa mi ndio nimeongoza chuo kizima ,haya hongera zako , halafu pia kuna suprise nataka nikupe mama yangu , ipi hiyo ,ni siri utaona baadae , haya, halafu mama , mmh nini tena , nina shida ya kiasi kadhaa cha fedha , nilijua tu wewe uache kuomba hela mtoto wewe kama ulizaliwa benki vile haya shilingi ngapi , kama laki tatu hivi , haya kesho, haya mama siku njema ,nawe pia masomo mema baba, haya kwaheri ,haya. Kwa mtoto wa mwalimu mkuu ilikua sio kazi kupewa laki tatu ni kama kuomba maji mtoni yani ilikua rahisi kweli kweli . Masomo yaliendelea na Martha alikua kidato cha nne wakati fulani akafunga shule na likizo hakwenda Mwanza kwani ilikua likizo ya muda mfupi kama wiki moja tu hapo alipata nafasi rasmi sasa ya kukutana na Vatican tena aisee Martha maharage ya shule yalimkubali alikua kanona ile mbaya alinenepa kwa kiasi kama ni ngombe basi hata wasingengojea sikukuu tayari angekua ameshachinjwa umbo lake mithili ya namba nane na alivyonawiri mweupeee Vatican alikosa cha kuongea ila cha kushangaza zaidi walipoonana hakuna aliyemsemesha mwenzake hapa ilitumika lugha ya matendo yani walicheka kila mmoja akitabasamu na kucheka kumvutia mwenzie ilikua kama sumaku vile huo mvutano yani ghafla kila mmoja alijikuta kwenye ndimi ya mwenzake wakaanza kubadilishana bacteria mwaaa mwaaa ndio sauti zilizosikika. Kubadilishana mate tu watu kidogo wajigonge wengine nao hadi wakaacha shughuli zao wakishangaa watu wanang'atana midomo bila kuumia Vatican hapo kakamatilia kiuno taratibu anashusha shusha mkono hadi kwenye makalio hahahahahaha ndivyo mambo ya vijana yalivyo ila sasa hili lilikua fumanizi ni Mary alitoka nje na kukuta Vatican na Martha wakifanya yao aisee ilimuuma sana na Mary hua akopeshi hapo hapo aliwafuata na kuanza kuongea mhhh haya wapendanao sasa mtauza sana sura mwaka huu sijui nawe umempendea nini gunia kama hili (huku akimwekea kidole usoni Martha) Martha kidogo atake kupigana ila Vatican akamzuia hawakuishia hapo kula raha bali walirudi tena JB Belmont kukumbushia raha za siku ile ya zamani huko kama kawaida yao hawakuacha kunywa na kula vya kutosha ila sasa Vatican alidhamiria kuvunja amri ya sita siku hiyo kwani alikazana sana kumshika shika Martha mapaja mara kumbusu sana kama aliyehitaji Mambo fulani hivi kutoka kwa Martha kwa kuwa ilikua ni the promise ilibidi Vatican awe mpole na kusubiri hadi siku ya ahadi itakapofika siku hiyo Martha alikua makini sana hakunywa pombe wala hakutaka kukaa sana kwenye starehe siku hiyo hivyo alirudi mapemaa nyumbani kisha wakaagana na kuachana kila mmoja alilala kwa furaha huku akimfikiria mwenzake ilikua ni kama ndoto na siku hiyo hakuna aliyelala kwa raha walizoponda siku hiyo kama mwenye njaa kutupwa katika msitu wa matunda. Likizo iliisha na Martha akarudi shule siku nazo hazigandi kama maziwa mtindi kujenga historia zaidi ya mwanamalundi sasa Martha alimaliza kidato cha nne sio yeye tu pia na Vatican naye alimaliza mwaka wa tatu chuo hivyo kama muda wa kutimiza ule usemi wa ahadi ni deni ulitakiwa utimizwe yani ni kuwasumbua wachawi kwa sauti za kuwafanya wasiloge usiku na kuwasikiliza nyie hahahahaha najua ulishatambua kama una nia ya kujua ni zile mechi muhimu zenye matokeo matatu tu kushinda kushindwa au kutoa sare tena zipo za uwanja wa nyumbani na zile za ugenini ila kubwa zaidi ni zile za kimataifa hapo uwanja wa taifa kuna heshima yake hapo we acha yani unalichezea taifa lako , tuachane na mbwembwe hizo tuje kwenye mahafali iliyofana sana ilikua ni mahafali ya Martha kumaliza kidato cha nne aisee haya mahafali yalikua ya kifahali watu walikula hadi wakawa wanaitwa warudie tena , mzee Adam alikuepo mama Martha Dayness na Mary kuchukua taarifa za umbea .Martha alipewa laptop kama zawadi kutoka kwa baba na saa ya dhahabu kutoka kwa mama , Vatican naye hakusita kupita japo kwa mbali japo alione ua la moyo wake kheri subuhana na radhi zake upendo huu uishe kwake aisee yani mvutano zaidi ya marhamu tamu inavyonukia huku Martha akinuia japo amuone hata kwa mbali Vatican naye alisubiri apate majibu ya asali asije umia kwa uchungu wa shubiri wakakutana wawili kama hadithi vile kidogo mambo yafanyike yakumtafuta mrithi ila aaah Vatican akajisemea sizitaki mbichi hizi " ishara ya upendo kuonyesha uvumilivu na skendo hatoi maulana uzuri wako bado msichana nakupenda tena nakupenda sana pindi uniachapo mi nitakazana niombe radhi kwako usije nihama atakayesema chokochoko ruhusa kumtukana" haka ni ka nyimbo ka msanii Joseph ambako Vatican alikua anakaimba huku kabeba  maua yake mawili kama ishara ya upendo na Martha kifuani mwake waliachiana na Martha akamuaga kwa busu hatari sijapata ona hadi watu walisikia kisha akarudi haraka kwa wazazi wake sherehe ikafana na ikawa kama historia mzee Adam hakutaka aaache kitu Martha alikua anaondoka naye kurudi nyumbani Mwanza huko atasubiri matokeo Martha alibisha kwanza kidogo baadae ikabidi akubaliane na baba yake na kurudi Mwanza Vatican naye hua ashindwi kitu si akarudi pia nyumbani kwao Mwanza sa hapo bila bila mzee Adam na Vatican . Milima haikutani ila binadamu hukutana, kwenye hoteli moja maarufu Mwanza ambayo wafanyakazi , mabosi na watu maarufu hukutana hapo kupata chai na chakula cha mchana hapo ndipo Irene kwa miaka zaidi ya mitano hivi anamwona tena Adam ila Adam ni baada ya miaka 25 anakutana tena na Irene aisee ilikua siku ya kazi jumatano Irene amekwenda kupata kifungua kinywa kama kawaida yake katika hoteli ile ila Adam yeye siku hiyo alipelekwa hapo na rafiki yake wa karibu sana na meneja masoko Humprey katika kampuni aliyokua anafanya kazi Adam ,lengo la Humprey ilikua ni kumkutanisha Adam na rafiki yake wa karibu wa Humprey ambaye katika tetesi Humprey alimwambia Adam kuwa angependa amuoe ila alikua bado akisubiri majibu kutoka kwa mama huyo. Kweli walitangulia wao kufika na kuagiza kile walichotaka Adam kwa shauku si akaanza , Humprey huyo mrembo mbona hafiki au umepigwa changa la macho hahahahaha na wazee unajua hua hatutaniani sasa kama ulitaniwa au leo siku ya wajinga nini ?, Aaaa Adam sipendi utani bwana haraka haraka haina baraka subiri atakuja uje umuone we mwenyewe utamkubali mama wa watu alivyoumbika. Kama unakumbuka zamani Adam naye alikua mtu wa wanawake hivyo sifa tu alizoambiwa na Humprey ye mwenyewe mate yakaanza anza , haikuchukua muda akafika 

0 comments:

Post a Comment