Sehemu ya 22
basi Dayness alikwenda na wazo la kuiokoa ndoa
yake aliwaza aende kukutana na Irene na kuongea naye kwani alihisi kuwa Irene
alikua chanzo cha mume wake kuwa hivyo . Kweli Dayness alifika nyumbani kwa
Irene na alikaribishwa na Vatican , hakujua kwamba Vatican alikua mpenzi wa
mtoto wake Martha kweli Dayness alikaribishwa ndani na kumkuta Irene , Vatican
aliwapisha waongee , Dayness akaanza ,dada huyo ni kijana wako , ndio kijana
wangu wa kwanza anaitwa Vatican kamaliza chuo mwaka huu bado yupo nyumbani
hajapata kazi si unajua ajira kwa vijana siku hizi ngumu , kweli kabisa dada ,
aisee samahani dada nimeshasahau utatumia kinywaji gani , hapana samahani wala
usihofu nipo sawa kabisa, usione aibu hapa ni nyumbani , hamna tabu sema tu
kuna jambo nataka kukuuliza dada , upo huru sema tu dada , nilikua nasema hivi naomba uwe mkweli dada sababu hili swala ni kubwa sana na na linahitaji
ukweli kwa kweli mume wangu siku hizi amechanganyikiwa kabisa tokea Humphrey
atangaze kukuoa mume wangu Adam kabadilika sana kitabia yani kama taarifa za
ndoa yako zilimuwehusha kabisa na mi kwa muda mrefu nilihisi mabadiliko kutoka kwa
mume wangu hakunipenda kama alivyonipenda zamani
haki ya ndoa ilikosekana hata na salamu pia baya zaidi ni pale alipojiunga na
unywaji wa pombe ndio akawa anarudi saa nane yani ndoa yangu iliteteleka sana
sana dada nimeumia sana hadi sasa hivi kazi kaacha dada kama unahusika kwa
lolote tafadhali naomba umuachie mume wangu niachie mume wangu nampenda sana
dada tafadhali Dayness aliongea hayo huku machozi yakimbubujika katika paji
lake jeupe la uso kama mtu angeweza kukinga kikombe basi machozi yale yalikua
mengi yangeweza kujaza jagi kabisa kisha baada ya kukaa muda mfupi akiwa kimya
Irene alimjibu, dada pole na samahani
sana kwa hilo ki ukweli mimi naomba nikueleze hivi huyo kijana unayemuona hapo
ni mtoto halali wa Adam anaitwa Vatican mimi na Adam tulikua wapenzi tulipokua
watoto kijijini tulipozaliwa Igombe kisha tukiwa bado tunasoma Adam alinipa
ujauzito na kisha akaniacha na kukimbilia mjini mimi huko kijijini shule
niliacha wazazi wangu na jamii ilinitenga nikaishi peke yangu na tumbo langu (
huku akilia)kwa kweli dada niliteseka nan niliumia sijapata kuona hadi pale
alipotokea msamaria mwema mzee Shaban aliyeahidi kunioa na kurudisha heshima
yangu hapo ndipo nilianza mwanzo mpya wa maisha yenye furaha mimi na mwanangu
kisha nilijiapia sitomtafuta wala kumwambia chochote Adam kuhusu taarifa zangu
na mtoto na yeye tangu akimbilie mjini hakuwahi kurudi mimi nilipohamia mjini
baada ya mume wangu kufariki na kuniachia urithi ulioniwezesha kuanza maisha
mapya huku mjini na ndio hadi sasa nipo hapa mara ya kwanza nakutana na Adam
alinishangaa na kisha kadri siku zilivyozidi kwenda aliniomba msamaha na
kunitamkia kuwa alikua bado ananipenda ila mi nilimkatalia na kumwambia kuwa
anaweza kuwa rafiki tu basi kwa ufupi ndio hivyo ,dada kumbe Adam ana mtoto mkubwa
hivi na hakuwahi kuniambia , pole sana dada hayo yalikua ya zamani , ila
madhara yake yanaonekana sasa hivi dada kumbe mimi ndio niliharibu mapenzi yenu
kwa kuingilia kati , hapana dada hapana , usifiche ni ukweli mtupu isingekua
mimi kuolewa na Adam angekua tayari ameshakutafuta na mngerudiana , hapana dada
achana na mawazo hayo we jaribu kumjenga mume wako kisaikolojia anisahau mimi ,
sasa nitafanyeje, mimi nitakusaidia kwa kuhama mji huu ili mume wako asiwe
ananiona , basi dada ni hayo tu mi naomba niondoke , jamani karibu tunapika ,
ahsante kwaheri, haya kwaheri. Dayness alipofika nyumbani akili yake ilimtuma
kuwa yeye ndio alikua chanzo cha yote hayo yani isingekua yeye Adam na Irene
wangekua hawana matatizo wala mapenzi yake yeye na Adam yasingekuepo na
asingeumia hivyo alijilaumu sana na kisha akachukua maamuzi magumu , chumbani
alipokuwapo alimuita Martha na kumuhusia mambo yote kuhusu mapenzi na mahusiano
kwamba hata siku moja asijaribu kuchukua mpenzi wa mtu mapenzi yanaua kisha
alimtuma Martha Juisi ya matunda na Martha alipoleta Dayness alimkumbatia
Martha kwa nguvu yapata dakika nzima huku akitokwa machozi Martha aliuliza kama
kuna tatizo na mama yake alisema hapana kisha Dayness alimtuma Martha sokoni
amfuatie matunda Martha alipotoka tu ndani na kuondoka Dayness alichukua sumu
ya unga ya panya na kuchanganya na juisi aliyokua nayo kisha akainywa
haikuchukua muda kufanya kazi Dayness aligaagaa huku na kule akihangaika chini
kwa muda kisha akatoa povu jeupe mdomoni na kukata roho maskini Dayness alijiua
0 comments:
Post a Comment