Sunday, October 11, 2015

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI 19

SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
SEHEMU YA 19

wewe kama mtu mzima ulishajua nini kilichoendelea hahahahaha jiongeze mkubwa hayo ndio yaliyoendelea huko. Vatican naye nyumba yake ilianza kuteteleka sijui ni sababu ya Irene baada ya kumuona yani mapenzi yake kwa Dayness yalianza kupungua muda mwingine hata kusalimiana ilikua tabu na haki ya ndoa ilipungua na kukosekana kabisa siku nyingine ilikua sio kama zamani alivyokua na mapenzi kwa mke wake maskini Dayness alihisi kuachwa kabisa ila kama kawaida ya wanawake hua hawaachi kufuatilia chanzo ni nini siku moja akamfuatilia mume wake anakwenda wapi siku moja Adam alimuomba Irene wakutane kuna kitu anataka kumwambia kweli kwa kuwa Adam alikua mzazi mwenzie Irene hakukataa kuonana naye na alijua ni kitu cha kawaida sana basi muda ulipofika kweli walikutana pale pale kwenye hoteli yao walipokua wanakutania Irene alikuja kwa muda muafaka waliopangiana wakutane kila mtu akaagiza huduma yake aliyoiitaji na kuanza maongezi Adam hakusita kuanza na salamu , za saizi , salama, habari za kazi , mmmmh ni nzuri, pole na kazi , ahsante , naomba radhi kwa kukupotezea muda wako , hapana wala haina shida kabisa kumbuka nilikuhakikishia kuwa utakua rafiki yangu hivyo sioni tabu au shida kuongea nawe, aaa basi sawa ila naomba hili jambo ninalotaka kukwambia ulichukulie umuhimu sana na unijibu ipasavyo , jambo lipi, kiukweli mimi nilikua napenda uniambie kama mwanangu ulijifungua au alikufa niwe na uhakika kabisa , Irene alikaa kimya kwa muda kisha akaguna kama aliyekua anavuta pumzi kusema kitu huku Adam akiwa amemkazia macho kujua Irene angesema nini na Irene akaanza kusema kwa sauti ya chini na kumwambia uliponiacha kijijini na ujauzito sio tu familia yangu kila mtu alinitenga na nikaishi mwenyewe sikuwa na wakunisaidia hivyo nilijifungua kwa shida na kwa bahati mbaya mtoto alifariki, pole sana , Irene alidiliki kudanganya huku akilia Adam kwa mapenzi mema alinyanyuka na kumsogelea Irene na kumkumbatia kama kumnyamazisha alipokua analia wakati Irene alifahamu kuwa anadanganya ila alijifanya mwenye majonzi huku akijiliza liza , Adam alimkumbatia Irene na kumbe Dayness aliyekua anamfuatilia mume wake kuwa wapi hua anakwenda ili ajue ni nani anayemuharibia mume wake hadi mapenzi yao yanapungua alifika , alipofika tu hakuamini alichokiona machoni kwake 

0 comments:

Post a Comment