sehemu 23
Dayness alichukua sumu ya unga ya panya na
kuchanganya na juisi aliyokua nayo kisha akainywa haikuchukua muda kufanya kazi
Dayness aligaagaa huku na kule akihangaika chini kwa muda kisha akatoa povu
jeupe mdomoni na kukata roho maskini Dayness alijiua. Ilikua huzuni majonzi na vilio kwa familia ya Mzee Adam ndugu jamaa na
marafiki wa karibu taratibu zote za mazishi zilifuatwa Dayness alizikwa . Irene
alipata taarifa za msiba ila hakuhudhuria kwani alijua kuwa maneno na ukweli
aliomwambia Dayness ndio ulimfanya ajiue kwa kujiona kuwa yeye Irene alikua ni
chanzo cha kifo Dayness hivyo ilibidi Irene aseme
ukweli wote kuhusiana na maisha yake na alianza na mwanae Vatican na alimwambia
hivi , mwanangu kuna kitu nataka kukwambia na naomba ukishike sana kwa kuwa ni
muhimu sana na unisamehe pale nitakapokuumiza hisia zako , mama ni nini tena
hicho naomba uniambie , ni kuhusu maisha yako na ukweli kuhusu baba yako ukweli
ni kwamba Marehemu mzee Shaban alale pema alikua mtu mwema na alikupenda sana
ila hakuwa baba yako mzazi , sasa mama mbona unanichanganya baba yangu mzazi ni
nani , huko ndipo ninapoelekea mnamo miaka 25 iliyopita baba yako mzazi
alinitelekeza na ujauzito wako kisha akakimbilia mjini mimi nilitengwa na jamii
nzima pamoja na wazazi wangu ila mzee Shabani pekee ndio aliniona na kunisaidia
kwa kunioa na kuwa mke wake wa tatu hapo ndipo maisha yangu yalinyooka na
kumsahau kabisa baba yako ila yupo na tupo naye hapa Mwanza anaitwa mzee Adam
ni muhasibu wa TBL ila sasa ana matatizo kidogo akiwa sawa nitakupeleka
ukamuone samahani sana mwanangu kwa kukuficha ukweli , hapana mama pole kwa
yaliyokukuta sikuyajua ila ukipata muda utanipeleka nikamuone, haya sawa baba.
Huku kwa mzee Adam mazishi yaliisha na kifo cha Dayness kilikua kama mwanzo
mpya katika maisha ya Adam kwani Adam sasa alimpenda mwanae alirudi kazini na
alijirekebisha tabia kwa kuacha pombe alijua kama mke wake angekuwepo angependa
mume wake awe na tabia nzuri za hivyo sasa ulikua ni upweke katika familia
nzima ya Mzee Adam ila kwa kuwa waliungana wawili yeye na mwanae waliishi kwa
amani upendo . Kisha Irene alichukua hatua kubwa zaidi ya kwenda kumwambia
Humphrey ukweli wote kuhusu maisha yake na mahusiano yake ya zamani na Adam huu
ulikua ni ujasiri wa hali ya juu hapo alikutana na Humphrey na kuanza kumwambia
hivi , habari yako Humphrey , nzuri tu mpenzi wangu habari ya kwako (huku
akiweka mkono begani kwa Irene) Irene aliutoa mkono na kisha kumwambia Humphrey
, nina kitu muhimu sana nahitaji kukuambia , kipi tena hicho au unataka tuoane
sa hivi, hapana sio hivyo ila ni kitu muhimu sana katika maisha yangu mimi
kabla ya kuwa nawe niliwahi kuwa na mpenzi na nilizaa naye mtoto mmoja ambaye
ninaye kama hufahamu hilo na baba wa mtoto huyo nininini ni rafiki yako kipenzi
Adam ndio alikua mpenzi wangu wa zamani na hadi sasa alikua bado ananipenda ila
mi nilimkatalia na kukukubalia wewe ilikua ni sababu ili nimuumize tu Adam na
kulipiza kisasi ila ki ukweli naomba msamaha kwa kuwa mimi sikukupenda kwa
dhati , Irene siamini kama unanitenda hivi kweli yani mi
niliamini nimepata mke wa kumuoa kumbe aisee kwa hiyo ndio tumeachana au yani
Irene ukiniacha unanikumbusha maumivu ya marehemu mke wangu , Humphrey mimi
kuwa na wewe haiwezekani kwa kweli yani ni kama kulazimisha pikipiki kuwa gari
naomba samahani sana , Irene alimuacha Humphrey na kuondoka zake dah Humphrey aliumia sana ila ndio hivyo
hakuwa na jinsi ya kufanya alijikaza kiume tu , huku kwa Martha zilitokea
dalili ambazo zilimshitua sana alianza kutapika na kujisikia vibaya hivyo
akaamua kwenda hospitali kujua nini kilimsumbua kiafya ndipo alipopata jibu
lililomshitua sio tu kiakili bali ilikua ni mabadiliko ya kimwili " umia
ujae " ndiyo kilichomtokea Martha alikua na ujauzito kama wa wiki zipatazo
mbili hivi aaaaaah aliona hata aibu kumwambia ukweli baba yake na baba mtoto
wake Vatican ilikua ni kipindi kigumu sana kwake ila bahati mbaya tumbo hua
halifichiki ndipo mzee Adam akaanza kuona dalili kisha akaamua kumuuliza ,
Martha mama njoo maramoja kuna kitu nataka kukuuliza , shikamoo baba , marahaba
habari yako , nzuri tu baba , ila mimi naona sio kama nzuri sana , kwa nini
unasema hivyo baba , mama naona mabadiliko sana katika mwili wako wala sio
unene huo hayo ni mabadiliko makubwa Martha mi sitakufanya chochote ila naomba
uniambie ukweli wote
0 comments:
Post a Comment