SIRI HUFICHULIWA NA MJASIRI WOGA UKIKITHIRI
SEHEMU YA 17
haikuchukua muda akafika Irene mamamamama pwaaaa
moyo wa Adam ulishituka alikua ni Irene yule yule mzuri vile vile kama zamani
alipokua na miaka 17 mwenye sura ya kupendeza mwili ambao kama ulitengenezwa
vile yani kama alikua bado binti kumbe mama wa miaka arobaini na kadhaa hivi
Adam alibaki ameduwaa kama aliyeshangaa mwonekano mzuri wa Irene ghafla
alishituliwa na sauti ya Humprey akimkaribisha Irene karibu mwalimu Irene ,
ahsante habari zenu, oooh salama salama Adam ,Adam unasalimiwa , Adam
alishituliwa na Humprey kwani alikua bado ameduwaa huku akicheka hahaha salama
tu mawazo haya, Humprey bila kuchelewesha muda akaanza utambulisho Adam huyu hapa anaitwa Mwalimu Irene ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi
kitangiri , ooooh nashukuru kumfahamu huku akimpa Irene mkono , Irene naye
akasita kidogo kisha akampa mkono Adam na Adam naye akatambulishwa kwa Irene ,
Irene huyu ni rafiki yangu kipenzi anaitwa Adam ni muhasibu mkuu wa TBL , oooh
nashukuru kwa kumfahamu alisema Irene. Kisha
Irene aliagiza chakula alichohitaji na kukaa Adam hakuacha kumtupia jicho Irene
kwa chini chini mwishowe kama ka mchezo wakawa wanatupiana macho kwa kuibia
mithili ya kutegeana yani huyu anamwangalia mwenzie kisha anapindisha macho na
mwenzake pia anamuangalia mwishowe hadi Humprey akataka kuwashitukia na
akauliza vp mnafahamiana au naona wote kwa pamoja wakaitikia aaaa hapana wala
hatufahamiani , aaah sawa nilidhani mnafahamiana. Adam alianza kukumbuka zamani
na kujiuliza kama Irene alikua mwalimu wa kitangiri basi ndio yule
aliyewasiliana naye kitambo kipindi mwanae alipopotea shule pia akaanza
kufungua simu yake na kutafuta namba ya Irene aliyoiifadhi miaka iliyopita
kwenye simu yake Mungu saidia akaipata bwana hapo hapo akaanza uchokozi ulikua
ni uchokozi wa kubip zaidi ya mara tatu akamudu kukatisha mazungumzo ya Irene
na Humprey ila Irene kwa kukomesha akazima kabisa simu hapo akamkomesha kabisa
kisha mazungumzo yao yakafana na kua vyema na sasa Humprey akapanga kutupa
nanga za kiutu uzima na hapa akaanza pole pole ki hivi sasa mwalimu
unalifikiriaje lile swala langu nililokugusia kipindi kirefu , jamani huniachi
hata nifikirie kidogo jibu lako nitakupa tu , haya ngoja nisubiri, Adam kwa
chini chini si akakaza macho kwa Irene hapo ndipo Irene alipochukua maamuzi
magumu ni ya kusogea karibu na Humprey kisha akamwekea mkono juu ya mabega yake
na kumwambia unajua nini Humprey unaonekana mwenye nia sana na mimi sasa naona
wacha nikupe nafasi japo nijaribu nione kwa sababu nyinyi wanaume hua
hamtabiriki mwanzoni mnaonyesha kama mna upendo kisha baadae mkipata
mnachokihitaji hukimbia na kutuacha wapweke (Irene alimaanisha hivyo kama
kumuumiza Adam kwa mafumbo) , aaah hayo mi siwezi kufanya mi bwana najua
kutunza wanawake wala sitokuumiza na utu uzima wangu kweli huu nifanye mambo ya
vijana hayo siwezi ,alisema Humprey , Huku Adam aliumia roho zaidi yale mapenzi
ya zamani kwa Irene alikua bado anayo na aliumia kuona Irene anakwenda kwa
Humphrey kiulaini kumbe Irene naye alifanya hivyo kumuumiza Adam asikie maumivu
aliyoyapata yeye miaka kadhaa iliyopita na kweli Adam aliumia kabisa sema
alijikaza kwa kuwa ilikua mbele ya rafiki yake. Kisha makutano hayo yaliisha na
kila mmoja alimuaga mwenzake na kuondoka ilikua ni furaha kwa Humphrey na kilio
kwa Adam na sasa Adam aliona acha ajaribu nafasi yake kwa kumpigia simu Irene ,
huku Irene akiwa na furaha kwamba kamkomesha Adam mara simu ikaita akapokea
haloo nanana ( Adam alipata kigugumizi ) naongea na
mwalimu Irene tafadhali , ndio mimi nikusaidie nini ,(Adam akakaza sauti kwa
kukalipia) nimesema sitaki ujinga nataka unionyeshe mwanangu na unileze ni kwa
nini miaka yote hiyo hupo hapa hukuwahi kunitafuta , wewe baba una wazimu
kwanza naongea na nani we unapiga simu tu na kuanza kufoka unamfokea nani hebu kama umekosea namba bora
ukate au useme we nani , (Adam kwa upole) aaaah samahani sana mi naitwa Mr Adam
ni menejaaa, wala hata usimalizie ehe shida yako nini ? Una wazimu hivi
ulidhani kuwa sitoishi uliponiacha na mimba yangu sasa umekosea njia mtoto wako
hutamjua wala hana jina lako niache na maisha yangu niishi kwa raha kwanza
nitamwambia rafiki yako kwamba unanisumbua , aaaaah basi basi yaishe Irene
tukutane basi tuongee yaishe mi naomba msamaha najua nilikuumiza ila nina
sababu zangu njoo tuongee nitakwambia ukweli wote , tafadhala tafadhali sana sitaki
unipotezee muda wako na uongo wako wa tangu zamani , hapana naapa kweli
sitatumia muda mwingi kukueleza naomba tafadhali , haya sawa wapi na saa ngapi,
mmmh ni pale lenana hotel saa kumi jioni nadhani utakua umeshamaliza kazi zako,
hayo hayakuhusu haya nitakuja, haya kwa he haloo haloo, kabla hajamaliza simu
ilikua tayari ilishakata , kesho yake muda ulipofika kweli baada ya kazi Irene
alikwenda Lenana Hotel pasiansi na kukutana na Adam, kwa mbwembwe kabla Irene
hajakaa Adam akamvutia kiti na kumruhusu akae kisha akamuuliza Irene angetumia
kinywaji gani na kuagiza, maongezi yakaanzishwa na Adam mwenyewe aisee siamini
japo miaka imekwenda Irene we bado ni mzuri vile vile na mrembo wa kuvutia kwa
kweli sichoki kukuangalia nikikumbuka zamani nilivyokupenda hadi moyo unaniuma
, eeeeeh wewe baba sikuja kwa hayo hebu eleza shida zako haraka mi niondoke
naona kama unanichelewesha , aaah samahani kwa hilo unajua tangu tuachane
kijijini sijaacha kukufikilia wewe yani upendo wangu kwako bado upo ule ule ,
(Irene huku akitaka kunyanyuka) wewe hebu usiniletee mambo ya kizamani historia
ambayo ilishafutika kichwani mwangu kama huna la kuniambia mimi naondoka , aaaa
basi basi najua unanichukia sana kwa mambo niliyokutendea ila naomba samahani
sana naomba msamaha kwa hilo Irene kuna sababu nyingi zilizonifanya kukuacha
kijijini , kama zipi , nyingi tu, hazina majina au kumbe nia yako ilikua
kunichezea na kukimbilia mjini , hapana hapana , ila , ila matatizo madogo tu ,
aaaah sawa hayo matatizo madogo ndio yananifanya na mimi nikuache sa hivi ,
usifanye hivyo usi , tayari Irene alinyanyuka na kutaka kuondoka Adam haraka
alimdaka Irene miguu na kuing'ang'ania kwa kuikumbatia huku akiwa kapiga magoti
na kichwa chake kipo usawa wa tumbo la Irene na akiwa kakiegemesha hapo akisema
naomba msamaha nisamehe tafadhali Irene , mwili wa Irene ulisisimka na hisia
zake zikamjia na kumrudisha mbali kumbuka ni miaka mingi hakuwahi kukutana na
mwanaume yoyote kimwili sasa mkono wa Adam uliopita kiunoni mwake uliamsha
hisia zake na kumkumbusha zamani sana kwa moyo wa hurumu Irene huku akiwa
amemshika Adam kichwani akasema unaniaibisha bwana tafadhali simama simama ,
Adam akajibu siwezi kusimama hapa hadi uniambie kama umenisamehe au , Irene
alisita kidogo na alipoangalia watu wote katika hoteli hiyo waliduwaa
wakiwaangalia wao kwa kuepusha aibu Irene ilibidi aeleweke tu na kusema haya
nimekusamehe simama sasa
Friday, October 09, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment